Wednesday, August 28, 2013

ZIFAHAMU FAIDA ZA KUFANYA MAZOEZI






Mazoezi ya viungo ni muhimu sana kwa afya yako, kuna namna mbalimbali za kufanya mazoezi. Unaweza kufanya mazoezi ya viungo fulani vya mwili wako kama miguu, mikono, mgongo nakadhalika. Lakini pia kuna mazoezi ambayo ukifanya utakuwa umefanya zoezi lilojumuisha kiungo zaidi ya kimoja mfano mazoezi ya kukimbia, kuruka kamba na mengineyo. Licha ya kuwa unaweza kutumia muda kidogo kufanya mazoezi kwa takribani dakika (30-45) kwa siku iwe asubuhi au jioni lakini pia unaweza kupata faida nyingi za kiafya kwa kufanya mazoezi hayo.

Kwakuwa kuna faida nyingi za kufanya mazoezi basi leo nimeona niorodheshe hizi chache kwa manufaa na ufahamu wa afya yako.
1. Mazoezi hukufanya uchangamke na kuwa shupavu.
2. Mazoezi huboresha ufahamu wako uwezo wa kuelewa na kufikiri mambo katika mazingira yanayokuzunguka.
3. Mazoezi huboresha uwezo wako wa kuhifadhi kumbukumbu.
4. Mazoezi husaidia kupunguza msongo wa mawazo.
5. Mazoezi huimarisha moyo hivyo hukuepusha na maradhi mengi yatokanayo na mapigo mabaya ya moyo.
6. Mazoezi humfanya mtu ajiamini.
7. Mazoezi hupasha mwili joto hivyo husaidia kuzuia baridi.
8. Mazoezi husaidia kuweka sawa kiwango cha cholesterol au mafuta yaliyopo mwilini.
9. Mazoezi hupunguza uwezekano wa mtu kupata ugonjwa wa kisukari.
10. Mazoezi hushusha kupanda kwa shinikizo la damu. (high blood pressure)
11. Mazoezi hupunguza uwezekano wa mtu kupata baadhi ya maradhi ya saratani.
12. Mazoezi humsaidia mtu kuondokana na baadhi ya matatizo ya akili.
13. Mazoezi huboresha hamu ya mtu kuweza kula.
14. Mazoezi hupunguza uzito wa ziada wa mwili na kufanya mwili wako kuwa mwepesi.
15. Mazoezi huimarisha mifupa hivyo hupunguza matatizo yatokanayo na kudhohofika kwa mifupa jina la kitaalamu (osteoporosis)
16. Mazoezi huboresha kinga ya mwili.
17. Mazoezi husaidia kuweka sawasawa mifumo mbalimbali ya mwili. Mfano: mfumo wa ufahamu, mzunguko wa damu, homoni na misuli.
Mpendwa msomaji hizi ni baadhi ya faida za kufanya mazoezi, yote ya yote mazoezi hurefusha maisha kwa kukufanya uwe mwenye afya njema. Ni vyema ukajiuliza, hivi ni kweli ukifanya mazoezi na kula vyakula bora kunaweza kuboresha maisha yako? Jibu ni NDIYO mazoezi na vyakula ni dawa pekee ya kutibu au kukuepusha na magonjwa mengi yanayoweza kuzuilika. Fanya mazoezi kuimarisha afya yako!

imeandikwa na saidi kamotta
ahsante kwa kutembelea blog hii
wako faraja mmasa a.k.a moa

usikose kitabu changu pale kitakapotoka


Share:

0 comments:

Post a Comment

KUHUSU MMILIKI WA BLOG HII

My photo
Naitwa faraja Mmasa a.k.a Moa,Mkazi na mzaliwa wa Wilaya ya Gairo Morogoro.KARIBU KATIKA BLOG hii tuelimishane mambo mbalimbali.Inatupasa kuwa na ufahamu wa mambo mbalimbali ili tuweze kuyatawala Mazingira yetu .Kuwa na Mwanasheria au Mhasibu haimanishi unatikiwa kujua au kufuatilia maswala ya uhasibu na sheria tu.Mfano nyumba yako au ndoa yako hutaindesha kwa taaluma uliyonayo.Vile vile huwezi kuendesha ujasiliamali kwa mafanikio kwa shahada yako ya uhandisi.TUNAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA

UJUMBE WA LEO

MIUJIZA MINGI INAYOTOKEA KATIKA MAISHA IPO KATIKA MAWAZO,FIKRA,NA IMANI ALIYONAYO MWANADAMU HUSIKA

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

GAR AD2

GAR AD2

GARI ADVERT

GARI ADVERT

Castrol

Castrol
Powered by Blogger.