Sunday, June 23, 2013

UNAFIKIRI UMECHELEWA KUFIKIA MAFANIKIO YAKO?


1.Unafikiri na kuamini kwamba huwezi kufikia vizingiziti vinavyokukwamisha  na unavyokutana navyo maishani?
2.Unafikiri na kuamini mafanikio hayawezekani tena?
3.Unafikiri muda umekutupa mkono kufikia malengo yako?
Kama majibu katika maswali yote hayo  matatu juu jibu ni  NDIYO basi soma kisa hichi chini ninachokwenda kukusimulia hapa chini kitakufanya ugundue mambo mengi maishani mwako ambayo ulikuwa huyafahamu hapo kabla.

Susan Boyle alizaliwa akiwa na matatizo ya ubongo  ambapo tatizo hili alilipata na kosa alilolifanya daktari wakati wa kuzaliwa kwake.Akiwa bado mdogo alijijengea tabia ya kupenda muziki kwa sababu hakua na mwonekano mzuri kutokana na tatizo alilokuwa nalo watoto wenzie wengi walimbagua hii ikapelekea yeye kujifariji kwa kupenda kusikiliza muziki. Familia yake ilikuwa ina matatizo makubwa kifedha yaani ilikuwa ni familia maskini. Mwaka 1995 alikwenda  kijiandikisha kwenye mashindano ya kutafuata vijana wenye vipaji vya kuimba lakini ALIKATALIWA  na majaji  wakamwona hawezi kitu.


SUZAN BOYLE
Pamoja na kukataliwa lakini suzan hakukata tama ya NDOTO yake ya kuwa msanii mkubwa ,lakini miaka miwili baadaye  baba yake akafariki dunia baada ya miezi michache dada yake akafariki dunia pia. Lakini pamoja na kupitia magumu yote  aliendelea na jukumu la kutimiza ndoto yake na HAKUKATA TAMAA!.
Mwaka 2007  mama yake mzazi aliyekuwa amebakia na ndie aliyekuwa msaada mkubwa sana kwenye maisha yake naye akafariki,Suzan  anasema AKAJIKUTA AMEBAKI PEKE YAKE DUNIANI.Baada ya mama yake kufariki suzani kwa mara ya kwanza akajikuta amekata tama katika uimbaji.
 Baada ya miaka mingi ya mihangaiko  na tabu  Suzan  akaamua tena kuanza kupigania kutimiza lengo lake na kwa mara ya kwanza akapata shindano lakuibua vijana wenye vipaji katika muziki na ndio shindano lilokuwa linaibua wanamuziki wenye vipaji nchini Uingereza.Suzan akapanda jukwaani kwa mara ya kwanza baada ya miaka 30 ya mihangaiko na tabu nyingi na vikwazo vya kila aina.
Siku chache tu baada ya suzan kupanda jukwaani na kuimba kwenye shindano lile ,video ya show yake ikawa alipokuwa jukwaani ikiwa ndio video iliyoonwa mara nyingi katika mtandao wa YOU TUBE. Suzan akawa maarufu Uingereza yote ndani ya usiku mmoja tu. Na albamu yake ya kwanza “ I DREAMED A DREAM”ikaongoza kwa mauzo nchini uingereza na ikashika namba moja katika chart zote kubwa Marekani.
Albamu yake ya kwanza tu ilimwingizia paund million 5 ambayo kwa Tanzania ni hela nyingi mno.Baadae akatoa albamu ya pili na ya tatu  nazo zikafanya vizuri sana. Mwaka 2012 utajiri wa Suzani unakadiriwa kuwa PAUNDI MILLION 30



UNAWEZA KUICHEKI VIDEO HII YOU TUBE KWA    LINKhttps://www.youtube.com/watch?v=RxPZh4AnWyk

KATIKA STORY HIO YA SUZANI TUNAJIFUNZA MAMBO YAFUATAVYO

1.MTU ASIYEJIWEZA AU MLEMAVU
Mtu mlemavu au asiyejiweza ni Yule ambaye ni mwenye afya njema hana tatizo lolote la kiungo cha mwili wake lakina anashindwa kupigana kutimiza MALENGO yake kwa sababu anaamini hawezi kuyatimiza.Sazani pamoja na matatizo aliyokuwa nayo  ya ubongo aliyoyapata wakati anazaliwa lakini amepigana mpaka kutimiza malengo yake.ndugu msomaji aacha kulalamika ka tatizo ulilonalo na kukata tama hata kama umezaliwa na tatizo flani la kiafya simama katika unachotaka kutimiza duniani hakika utafanikiwa.

2.SIKU ZOTE KUNA TUMAINI
Suzan alikuwa mlemavu  ,alikataliwa kila sehemu aliyokwenda,na akapoteza wazazi wote na ndugu zake lakini alikuwa na TUMAINI ipo siku atatimza tu malengo yake,popote kwenye tumaini hakuna kinachoshindikana

3.HAKUNA KITU KUCHELEWA KWENYE MAISHA
Suzan alianza kuanza kuimba akiwa na miaka 12 lakini alikuja kujulikana akiwa na miaka 47.Ukiwa na nia na lengo unaweza kuanza wakati wowote lakini bila kukata tama na kujaribu kadri uwezavyo basi unaweza kufikia malengo yako maishani.

4.USIACHE KUJARIBU
Usiache kujaribu kadri uwezavyo jaribu mara nyingi uwezavyo,vipi kama suzani asingeenda tena kujaribu baada ya kukataliwa mara nyingi kabla ya kukubaliwa?tujaribu kadri tuwezavyo.

Ahsante sana ndugu msomaji kwa kusoma hio story hapo juu nafikiri umejifunza mambo mengi hasa kwa namna gani unaweza kufikia malengo yako maishani.
Wako mchumi faraja mmasa
UNAWEZA KUSOMA MADA ZAIDI ZA SAIKOLOJIA KWA KUPERUZI PAGE YA SAIKOLOJA NA MASHA KATIKA BLOG  HII AU BONYEZA HII LINK http://mchumifaraja.blogspot.com/p/saikolojia-na-maisha_07.html


“Tujitahidi kutenda mema kumbuka dunia hii tunapita,piga picha na wewe kuna siku ya kuja kubebwa na kuachwa kwenye makazi yako ya milele,jiulize kutokana na imani yako inakuambia nini,je wapi utakwenda baada maisha yako ya kidunia?”
Share:

"Mlee mtoto katika njia impasayo, naye hataiacha hata atakapokuwa mzee."

"
Habari za leo ndugu msomaji wa blog hii ya mchumi faraja mmasa,natumani ni mzima wa afya njema. Leo nimeamua kukuletea mada hii ili tuweze kupata mawili matatu katika malezi ya watoto sisi kama walezi,wazazi.mada hii ya leo ipo kidini zaidi hasa imeleemea katika upande wa wakristo ,lakini hata waislamu wanaweza kuisoma pia.Dhumuni la kuwaletea mada hii ni hasa kuwalea watoto wetu kiimani zaidi na kimaadili toka wanapokuwa watoto wadogo,kama tunavyoona hivi sasa dunia imechafuka,kama tukishindwa kuwalea watoto katika maadili ya kidini basi dunia ya hivi sasa ya utandawazi itawameza,naomba ufuatilie mada hii mpaka mwisho naamini kama mzazi au mlezi mpaka mwishoni utakuwa umejfunza kitu

Kumlea mtoto maana yake ni nini ?
Ni kumtunza na kumfundisha/kumuelimisha mpaka afikie mahali pa kujitegemea mwenyewe.
 Ni kumtunza na kumfundisha kwa vitendo na maneno mpaka awe mzima, kiakili na kiutu kiasi cha kuweza kuendelea mwenyewe bila ya kukutegemea.


Njia ipasayo kumlea mtoto ni ipi?

Ni njia ile nzuri yenye maadili mema yanayokubaliwa na Neno la Mungu pamoja na jamii unayoishi katikati yake.
Mwenendo wenu ni fundisho kubwa kabisa mbele ya mtoto wenu. Njia ipasayo kumlea mtoto ni kuketi na mtoto na kumshauri maadili mema ya maisha (Kumb 6:7). Ni kumwelekeza kwenye mambo matakatifu, kabla hajaharibiwa na walimwengu.



Kwa mfano:-
Pale Nyumbani: Mlee mtoto katika njia impasayo naye hataiacha hataatakapokuwa mzee.
- Ibada za nyumbani kwa wazazi pamoja na mtoto/watoto ni kitu muhimu sana.
- Mazungumzo yenu yanayohusu watu wengine, majirani, watumishi wenzako nk.
- Mnavyojibizana na mkeo/mumeo mbele ya watoto na hata sura yako ya kila siku mbele za watoto.
- Unavyowaelekeza watoto wako kuhusu maadili mazuri kwa waliomzidi umri.
- Adabu na heshima mezani mkiwa peke yenu na watoto au mbele ya wageni.
- Ikiwa wewe ni omba omba kila wakati hata watoto wako watakua hivyo.
Mahudhurio ya ibada:
 Mlee mtoto katika njia ipasayo naye hataiacha hata atakapokuwa mzee.
- Unatarajia mtoto atachukua fundisho gani ukibaki nyumbani wakati wa ibada?
- Unatarajia mtoto atajifunza nini kama kila siku unachelewa ibada na kuwahi kutoka au kukaa nje ya kanisa saa ya mahubiri?
- Unatarajia mtoto atajifunza nini kama huchukui Biblia wala kitabu cha nyimbo unapoenda ibadani?
- Unatarajia kuelewekaje unapowaacha watoto nyuma wakati unapokwenda kuhudhuria vipindi mbali mbali vya ibada?
Tunapokuwa ibadani:
 Mlee mtoto katika njia ipasayo, naye hataiacha hata akiwa mzee.
- Usimwache mtoto acheze cheze na kutembea hovyo wakati wa ibada huku akipiga makelele.
- Sio vema wakati wa utoaji wa sadaka kumpa mtoto senti 20 au 50 wakati unazo pesa zaidi ya hizo. Au kukaa tu bila kutoa sadaka wakati unapofika wa kutoa sadaka.
- Sio vizuri kupiga usingizi wakati ibada inaendelea. Au kutafuna pipi au “gum“ na kuchafua kanisa.
Kumbuka unayomfundisha mwanao kwa vitendo, yaweza kuwa picha nzuri au mbaya ambayo kwake itakuwa vigumu sana kuisahau au kuiacha hata atakapokuwa mzee!!!

Kwa nini?
Mzazi ni mwalimu wa kwanza kabisa kwa mtoto. Hivyo kila utakalomfundisha mwanao:-
- Atalizingatia na kulishika siku zote za maisha yake. Mfano: kama unapenda nyimbo za “dance“ au za kidunia yeye naye atazipenda hizo.
- Yale anayoyaona kwako anajifunza na kuyatendea kazi. Kwa mfano, kusema uongo, kuahidi bila kutimiza ahadi, kutukana nk
- Ukifanya kazi au kuishi katika hali ya uvivu usishangae mtoto wako akiwa mvivu.
- Ukiwa na bidii au ulegevu katika mambo ya Mungu, mtoto wako atakuwa hivyo.
- Ukiwa na hali ya usengenyaji na kuwadharau wengine mtoto wako atayaiga hayo.
- Kama una kiburi na majivuno au hali ya kutokumtii mumeo au kumpenda mkeo mtoto atajifunza hali hiyo.
- Kama una hali ya kutokuwa na ibada za nyumbani na uvivu wa kushiriki vipindi kanisani, mtoto atayaiga hayo.
- Kama unashabikia ya dunia na kuweka kando mambo ya kiroho mtoto atakuwa hivyo.
Hivyo mlee mtoto katika njia impasayo naye hataiacha hata atakapokuwa mzee.



TUWE VIELELELEZO VIZURI KWA WATOTO WETU NAO WATAKUA HIVYO.
SOMO HILI LIMECHAMBULIWA NA MCHUNGAJI MARANDU
AHSANTE SANA KWA KUTEMBELEA BLOGU HII
UNAWEZA SOMA ZAIDI KUHUSU MADA ZA MALEZI KWENYE PAGE YETU YA WAZAZI KATIKA BLOG HII KWA KUBONYEZA LINK HIIhttp://mchumifaraja.blogspot.com/p/wazazi_4.html

WAKO MCHUMI FARAJA MMASA
Share:

KUHUSU MMILIKI WA BLOG HII

My photo
Naitwa faraja Mmasa a.k.a Moa,Mkazi na mzaliwa wa Wilaya ya Gairo Morogoro.KARIBU KATIKA BLOG hii tuelimishane mambo mbalimbali.Inatupasa kuwa na ufahamu wa mambo mbalimbali ili tuweze kuyatawala Mazingira yetu .Kuwa na Mwanasheria au Mhasibu haimanishi unatikiwa kujua au kufuatilia maswala ya uhasibu na sheria tu.Mfano nyumba yako au ndoa yako hutaindesha kwa taaluma uliyonayo.Vile vile huwezi kuendesha ujasiliamali kwa mafanikio kwa shahada yako ya uhandisi.TUNAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA

UJUMBE WA LEO

MIUJIZA MINGI INAYOTOKEA KATIKA MAISHA IPO KATIKA MAWAZO,FIKRA,NA IMANI ALIYONAYO MWANADAMU HUSIKA

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

GAR AD2

GAR AD2

GARI ADVERT

GARI ADVERT

Castrol

Castrol
Powered by Blogger.