Friday, July 19, 2013

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU DAWA AINA YA 'DICLOFENAC' ILIYODAIWA KUWA NA MDHARA MWILINI.


1.Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) ina jukumu la kulinda na kudumisha afya ya jamii kwa kuhakiki ubora, usalama na ufanisi wa vyakula, dawa, vipodozi na vifaa tiba.


2. Hivi karibuni, TFDA imepokea taarifa ya kuwepo kwa hofu juu ya usalama wa dawa aina ya Diclofenac kupitia mitandao ya simu na vyombo vya habari. Kufuatia taarifa hiyo, TFDA inapenda kutoa ufafanuzi kama ifuatavyo:

 magonjwa mbalimbali. Magonjwa hayo ni pamoja na magonjwa ya viungo, mifupa, uvimbe wa fizi na maumivu ya kichwa.


b. Mamlaka imesajili dawa ya Diclofenac kutoka makampuni mbalimbali ndani na nje ya nchi baada ya kutathmini ubora, usalama na ufanisi wake. Hata hivyo Diclofenac, kama ilivyo kwa dawa nyingine, ina madhara yanayofahamika. Kwa baadhi ya wagonjwa Diclofenac inaweza kusababisha vidonda vya tumbo, kuumwa kichwa, kuharisha, kutapika na kuwashwa mwili.


c. Pamoja na madhara yaliyoainishwa hapo juu, hivi karibuni imetolewa taarifa na Mamlaka ya udhibiti wa dawa ya nchi za Umoja wa Ulaya (European Medicines Agency) kwamba watu wenye matatizo  ya moyo na shinikizo la damu, kisukari, waliowahi kupata kiharusi, wenye lehemu (cholesterol) nyingi kwenye damu, mshituko wa moyo na wanaovuta sigara wanaweza kupata matatizo kwenye moyo na mfumo wa damu ikiwa watatumia Diclofenac kwa kiwango kikubwa na kwa muda mrefu.


3. Kufuatia taarifa hiyo, TFDA inaendelea kufuatilia madhara yatokanayo na dawa hii kwa kushirikiana na taasisi nyingine za kitaalam ndani na nje ya nchi ikiwa ni pamoja na Shirika la Afya Duniani (WHO). Aidha, tunawakumbusha watoa huduma za afya kutoa taarifa za madhara yatokanayo na matumizi ya dawa kwa kujaza fomu maalum zinazopatikana katika vituo vyote vya afya nchini.
4. Mamlaka inasha+uri watoa huduma za afya nchini na wagonjwa kuchukua tahadhari za madhara haya hasa kwa watu wenye magonjwa ya moyo, shinikizo la damu, kisukari, wenye lehemu nyingi kwenye damu na wanaovuta sigara ikiwa ni pamoja na kutumia dawa mbadala.



5. Vilevile wananchi wanashauriwa kuepuka matumizi holela ya dawa bila kupata ushauri wa kitaalam ili kuepuka madhara yanayoweza kujitokeza.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) – Makao Makuu
S. L. P 77150
Dar-es-Salaam
Tanzania
Simu: +255 22 2450751
+255 22 2450512
Barua pepe: info@tfda.or.tz
Share:

NAMSIHI JANUARY MAKAMBA AACHE SIASA KATIKA SUALA LA KODI YA UMILIKI WA KADI ZA SIMU - MNYIKA


Kwa mliotaka msimamo wangu juu ya kauli ilinukuliwa jana tarehe 18 Julai 2013 na Gazeti la Majira kwamba Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia January Makamba kwamba “Mnyika anaangalia upepo unakoelekea, akiona watu wanalalamika ndipo anaongea namsihi aache kufanya siasa katika jambo hili”, naomba kutumia mtandao huu kutoa majibu ya ujumla kwa maswali na masuala yote kama ifuatavyo:

Nieleze kwamba sitaacha kufanya siasa kwenye jambo hili mpaka kodi hiyo itakapofutwa kuwawezesha wananchi wa kipato cha chini kubaki na fedha walau kidogo kwa maendeleo.


Sitaacha kufanya siasa kwa sababu ndio kazi yangu ambayo wananchi walinichagua kuifanya ya kuwawakilisha na kuisimamia Serikali ambayo yeye Makamba ni sehemu yake. Sitaacha kufanya siasa kwa sababu Mwalimu Nyerere alisema ili nchi yetu iendelee inahitaji watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora.
Share:

Wanamuziki 8 wa Marekani wenye majina ambao wameenda shule. (shule muhimu hata kama una kipaji cha usanii, zingatia)



1. Christopher ‘Ludacris’ Bridgesis (GA State University, Music Management)
2. Dwayne Michael Carter Jr. aka Lil Wayne (University of Houston, Political Science)
3. Common (Florida A&M University, Business Administration)
4. 2 Chainz (Alabama State University, Music)
5. David Banner (Southern University in Louisiana, Business Administration. University of Maryland, Masters degree in Education)
6. Jermaine Cole a.k.a J. Cole (St. John’ University, New York. Graduated with top honors)
7. Talib Kweli (New York University, Theatre Arts)

8. Sean Combs a.k.a P. Diddy or Puff Daddy (Howard University, Music).


source masanja@fb


Share:

TUSIPENDE KUJENGA CHUKI KWA KUWA TUNATOFAUTIANA KIMITAZAMO,KIHSIA,KIFIKRA,KITABIA!

KATIKA maisha yetu bila shaka tuna watu wengi au wachache ambao toka moyoni mwetu tunawachukia na pengine tamaa yetu ni kuona wanapatwa na mabaya kila siku. Miongoni mwao ni watoto, wazazi,waume, wake na ndugu zetu.

Pamoja na kuwepo kwa chuki ya asili ambayo nayo hufanya kazi kwenye maisha ya mwanadamu, lakini wengi wetu tuna chuki zinazotokana na orodha ya mabaya tuliyowahesabia wenzetu.

Mume anaweza kuwa na orodha ndefu ya matendo machafu ya mkewe tangu walipooana miaka saba iliyopita, ambapo kila siku anapomtazama tu huwa kama anatazama CD ya matukio yaliyopita na kuifanya chuki yake kukuwa kila siku.

Kwa bahati mbaya, wanadamu wengi wako hai kwenye mabaya, uwezo wao wa kukumbuka makosa ni mkubwa zaidi kuliko wema wanaofanyiwa. Tabia hii inatokana na ukweli kwamba, akili zina tabia ya kukosoa muonekano na taarifa ya vitu, lengo ni kuweka ulinganifu wa jinsi mtu anavyojitambua.

Share:

HEART TOUCHING STORY

I saw Amos in 1998 when i had left campus. I was workingin a supermarket in our local town.
           
At first i was not attracted to him but he was a kind of tall,Kind, gentle and mid sized youngman. Indeed he washandsome and sooner or later, i felt attracted to him.Our first days were good and he gave me everything ineeded.

He supported with my little salary though he was also notearning very much money and could provide me with rent,clothing and many times he gave me food.

One day, we were going out, he came picked me and wewent to the nearby resort. We enjoyed and he saw metalking to a boy who was my ex boyfriend outside the hotel,when i saw him watching me i felt so guilty and fearedapproaching him.

But when i approached him, he smiled at me and pretendedas if it was ok. I wondered what a kind of a man he was theone who smiled in every situation.
Share:

HEART TOUCHING STORY



A very poor man lived with his wife.

One day, his wife, who had very long hair asked him to buy her a comb for her hair to grow well and to be well-groomed.

The man felt very sorry and said no. He explained that he did not even have enough money to fix the strap of his watch he had just broken.
She did not insist on her request.

The man went to work and passed by a watch shop, sold his damaged watch at a low price and went to buy a comb for his wife.

He came home in the evening with the comb in his hand ready to give to his wife.

He was surprised when he saw his wife with a very short hair cut.

She had sold her hair and was holding a new watch band.

Tears flowed simultaneously from their eyes, not for the futility of their actions, but for the reciprocity of their love.

MORAL: To love is nothing, to be loved is something but to love and to be loved by the one you love,that is EVERYTHING. Never take love

for granted
Share:

NI NAMNA GANI TUNAWEZA KUFANYA YASIYOWEZEKENA

Ninatumaini ni mzima wa afya njema,karibu na nakupongeza kwa kuitembelea  FARAJA MMASA BLOG,naamini mpaka mwisho wa Mada hii utakuwa umepata kitu kipya na mtazamo  mpya wa maisha.


Kabla ya mwaka 1968 dunia nzima iliamini hakuna mtu anayeweza kuruka juu zaidi ya futi 28,lakini ilipofika mwaka 1968 mtu mmoja aliyeitwa Bob Beamon alikataa kuamini hivyo ni kitu kisichowezekana kuvunja na kuweja rekodi ya kuruka juuu zaidi ya futi 29,lakinibaada ya mazaoezi magumu na kujituma alivunja na kuweka rekodi ya kuruka futi 29.Kabla ya hapo dunia nzima ilikuwa na imani hakuna atakayevunja rekodi kabla ya Bob Beamon kuwanonyesha walikuwa wakiiamini kitu ambacho sio sahihi kwasababu alikataa kuishi kwa kuamini haiwezekani.
Lakini kitu cha kuchekesha na kustajaabisha kwa muda wa miaka 23 watu waliendelea kuishi na kuamini hakuna atakayevunja rekodi hio ya kuruka futi 29 aliyoiweka Bob Beamon na ndipo alipotekea Powell na kuruka futi 31.Lakini lazima ileweke pale mtu anapovunja rekodi basi mamia ya watu watatokea na kuvunja rekodi hio.
Lakini kwanini watu wanafanya miujiza kama hii au wanaweza kufanya mambo yasiyowezekana.

HIVYI NDIVYO UNAVYOWEZA KUFANYA YASIYOWEZEKANA
Imeeleweka kutoka kisa hicho hapo juu kwamba mambo yote tunayoshindwa kufanya ni kutokana na VIKWAZO YA KISAIKOLOJIA ZAIDI.Pale mtu anapoamini kitu fulani anaweza kufanya basi hata kama hicho kitu hakiwezekani mtu huyo anaweza kukifanya hicho kitu,ni tatizo zaidi la kisaikolojia linalofanya watu kushindwa kufanya mambo yasiyowezekana.Hata wewe hapo ndugu msomaji mara nyingi unapowaambia watu unataka kufanya jambo fulani ambalo watu wameshindwa kulifanya watakwambia huwezi wengi walijaribu na walikuwa na uwezo wameshindwa ije kuwa wewe.Ninaposeama ni vikwazo vya kisailojia namaanisha kwamba ni kwamba pale mtu anapofikia kikomo cha kuamini hawezi kufanya jambo Fulani wakati anauwezo wa kulifanya na kufanikiwa tena kwa mafanikio makubwa.



NJIA ZA KUFANYA YASIYOWEZEKANA
1.Kwanza amini wote waliofanya kabla kuna sehemu walikosea
Ili kuweza kufanya kitu ambacho watu hawajawaji kukifanya au wamekifanya lakini wewe unataka kukifanya kwa zaidi lazima ujiwekee akilini kuna kitu walikuwa hawajafanya kwa usahihi ni WEWE tu unayeweza kulitimiza hilo.
2.Pili, lazima uje vikwazo vyote ni vya kisaikolojia tu na sio kitu kingine
Vikwazo vyote ambavyo sasa vinakuzuia kufanya kitu ulichodhamiria jua ni vikwazo vya kisaikolojia tu,lakini pale utakapotambua ukweli tu na kukataa hichi kikwazo basi unaweza kufanya lolote lile ulilolidhamiria.
3.Tatu.ni lazima ufanye kitu( do something)
Kuamini kwamba unaweza kufanya yasiyowezekana hio ni hatua ya kwanza ,huwezi kufanya yasiyowezekana kwa kusema na kuamini tu, lakini ni lazima ufanye kitu ni lazima imani yako uiweke katika utekelezaji kama tunavyoambiwa katika vitabu vyetu vitakatifu imani pasipo matendo imekufa.Ngoja nikupe mfano mmoja wa bwana mmoja alikuwa anaitwa JOE WE unaamini unaweza kufanya miujiza hata kama huna rasimali za kutosha? .Kulikuwa na bwana mmoja anaitwa JOE alikuwa ana aibu sana na halikuwa hapendi kuongea na watu asiowafahamu au ambao amekutana nao kwa mara ya kwanza,lakini pamoja na hio JOE alikuwa na malengo makubwa siku moja atakuja kutoa motivational speech mbele ya watu maelfu kwa maelfu,lakini alikuwa anajua ni kitu ambacho hakiwezekani kwake,siku moja akaamua kuandaa speech na kuiwakilisha mbele ya rafiki zake lakini mwanzo wa kutoa speech tu akaishiwa na pumzi na kusahau karibia kila kitu alichokuwa amekisoma mwanzo mwishoni akaamua kuacha kutoa speech,lakini JOE alikuwa sahihi kuacha kutoa speech kwasababu alijua nafanya kitu ambacho hakiwezekani. Kwanini JOE alishindwa? Kwasababu ya mawazo ya muda mfupi na mipango ya muda mfupi,kama  angekuwa na mipango ya muda mrefu na kwa rasilimali alizonazo baada ya mwaka au miaka miwili basi angeweza kufikia lengo lake.
4.Acha kulia kama huna rasilimali za kutosha
JOE na watu kama joe huwa wanashindwa kufanya yale wanayoyataka kufanya kwasabu wananadharia za uongo kuhusu maisha kwasababu wanafikiria unatakiwa uwe na rasilimali zote  kwa kipindi wanachotaka kufanya yale waliyodhamiria la sivyo basi wangeacha kufanya yale waliyoyapanga kuyafanya maishani,lakini kwa kifupi kama unashindwa kufanya yale unayoyataka kuyafanya maishani kwasababu huna ujuzi basi ni vizuri kuanza kujifunza huo ujuzi kwa kiwango unachoweza taratibu mpka pale utakapofikia lengo kama joe alishindwa kwa sababu

kuna ujuzi alitakiwa kujifunza kwanza .Ninaposema rasilimali naamanisha mambo mengi ikiwemo ujuzi,fedha,muda na vinginevyo.
5.Usiwe na mawazo ya muda mfupi.
Joe alitaka kufanya yasiyowezekana ndani ya WIKI MOJA.Maisha sio rahisi hivyo kama una malengo makubwa na kutaka kufanya yale yasiyowezekana.Kumbuka yasiyowezekana ndani ya muda mfupi yanawezekana ndani ya muda mrefu,usiwaze kwa ukaribu na usiwe na mipango ya muda mfupi.

Asante kwa kutembelea blog
Wako
Mchumi faraja mmasa a.k.a moa.


*************Tujitahidi kutenda mema dunianai tunapita*************
Share:

FAHAMU Album Kumi Bora Wiki Hii Ndio Hizi





1] Jay Z - Magna Carta... Holy Grail

2] Ciara – Ciara


3] J Cole - Born Sinner
 
4] Florida Georgia Line - Here's To The Good Times


5] Imagien Dragons - Night Visions
 

6] Kanye West - Yeezus


7] Wale - The Gifted


8] Skylar Gray - Don't Look Down
 

9] Daft Punk - Random Access Memories


10] Macklemore & Ryan Lewis - The Heist
Share:

KUHUSU MMILIKI WA BLOG HII

My photo
Naitwa faraja Mmasa a.k.a Moa,Mkazi na mzaliwa wa Wilaya ya Gairo Morogoro.KARIBU KATIKA BLOG hii tuelimishane mambo mbalimbali.Inatupasa kuwa na ufahamu wa mambo mbalimbali ili tuweze kuyatawala Mazingira yetu .Kuwa na Mwanasheria au Mhasibu haimanishi unatikiwa kujua au kufuatilia maswala ya uhasibu na sheria tu.Mfano nyumba yako au ndoa yako hutaindesha kwa taaluma uliyonayo.Vile vile huwezi kuendesha ujasiliamali kwa mafanikio kwa shahada yako ya uhandisi.TUNAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA

UJUMBE WA LEO

MIUJIZA MINGI INAYOTOKEA KATIKA MAISHA IPO KATIKA MAWAZO,FIKRA,NA IMANI ALIYONAYO MWANADAMU HUSIKA

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

GAR AD2

GAR AD2

GARI ADVERT

GARI ADVERT

Castrol

Castrol
Powered by Blogger.