Wednesday, August 28, 2013

UMEKOSA FURAHA MAISHANI? HIZI MBINU ZITAKUSAIDIA KUWA NA FURAHA MAISHANI HAIJARISHI UPO KATIKA HALI GANI!-PART 2


Habari za leo ndugu msomaji wa blog hii ya FARAJA MMASA BLOG.Natumaini wewe ni mzima wa fya njema,leo naendelea na sehemu ya pili ya mada hii ,kama hujasoma sehemu ya kwanza ya mada hii bonyeza hii link UMEKOSA FURAHA MAISHANI? HIZI NI NJIA ZIKAZOKUSAIDIA KUWA NA FURAHA-PART 1

  5.JITAHIDI KUSAMEHE KADRI UWEZAVYO

Tafiti mbalimbali zilizofanywa na wanasaikolojia zinaonyesha,kusamehe husaidia kufanya msukumo  wa damu kuwa sawa na huweza kuzuia presha ya kupanda,vilevile jambo kubwa zaidi huweza kumuondolea mtu msongo wa mawazo unaoambatana na vinyongo kama mtu ana vitu vingi ambavyo hataki kutoa msamaha,hivyo kusamehe humfanya mtu kuondokana na stress na hivyo kumfanya mtu kuwa na furaha na kujisikia huru,pia kusamehe humfanya mtu kupata usingizi mnono,kuweza kuzuia hasira zisizokuwa na maana yoyote na hivyo kujiepusha na mitafaruku mbalimbali hivyo humfanya mtu maisha yake kuwa ya furaha muda mwingi
Mahatma Gandhi said, “Hate the sin, love the sinner.” and “The weak can never forgive. Forgiveness is the attribute of the strong.

6. JITAHIDI KUWA NA MARAFIKI WENGI
Mwaka 2010   utafiti uliofanywa na chuo kikuu cha Harvard  ulionyesha kwamba watu wenye marafiki wengi  huwa na furaha zaidi kuliko wale wenye marafiki wachache au wasio na marafiki kabisa,mara nyingi mtu asipokuwa na marafiki huwa mpweke na hivyo mara nyingi kujikita katika hali ya mawazo lakini pia anapopata tatizo hukosa watu wa karibu wakuweza kubadilishana mawazo na kuweza kutatua tatizo,lakini pia ni vizuri zaidi kuwa na marafiki ambao unaendana nao kimtazamo na kihisia na kiimani pia.Tafiti pia zilizofanywa  ziligundua unapojumuika na watu ambao mnaendana kwa kila kitu kwa asilimia kubwa furaha huwa ni ya kiwango kikubwa,hii ni kwasababu unapokutana na watu mnaoendana kwa vitu vingi  basi endorphin na dopamine neurotransimitters ambazo zinahusika na furaha huachiwa katika mwili,na hivyo kumfanya mtu kuwa na furaha zaidi.

7.ACHA KULAUMU KILA KITU NA KILA MTU NA KUJIONA UPO SAHIHI KWA KILA KITU
Wakati mwingine huwa tunakosa furaha maishani mwetu kutokana na tabia zetu za kujiona tupo sahihi kwa kila kitu ,jua kabisa kama wewe ni mwanadamu lazima  unamapungufu,mtu anapokuwa kinyume na jinsi wewe unavyotaka basi usijenge chuki,kikubwa zaidi jitathimin ikwa undani zaidi tatizo liko wapi,watu wengi huwa wanakosa kuwa na furaha sehemu za kazi kutokana na tabia hii ,kwa kuona kila mtu anayemkosoa ni mtu mbaya kwake .Unaweza kuwa unaelimu kubwa,una hela nyingi kuliko wengine,ni mzuri sana kwa ujumla umebarikiwa mambo mengi lakini haimanishi wewe ni bora kuliko wote,hizo sifa zote zinakufanya kuwa wewe tu,everyone is different,kwa hiyo kubali utofauti uliopo. Appreciate the differences instead of the shortcomings and you'll see people—and yourself—in a better light

8.JITAHIDI KADRI UWEZAVYO KUJITOLEA KWA AJILI YA WENGINE.
Shirikiana kwa hali na mali na watu wengine, huwezi kuishi mwenyewe hata kama una pesa, mali, chakula na kila kitu unachodhani ukiwanacho utakaa mbali na walimwengu. Dunia ya sasa inajengwa kwa kushirikiana hivyo ukitaka kufanikiwa na maisha yako penda kushirikiana na wenzako na kila kitu utapata kutoka kwa kwao. ''You receive more by giving more.'' Jinsi unavyojitolea kusaidia watu wengine ndivyounavyoongeza idadi ya watu muhimu kwenye maisha wako watakaokuwa msaada mkubwa kwenye maisha yako,na hivyo kuweza kukusaidia kwa namana moja au nyingine kufikia mafanikio au malengo yako na hivyo kuwa na furaha kwa yale unayoyafanya ,hata hivyo  ni jambo zuri na lenye furaha zaidi kujiona wewe ni mtu muhimu katika jamii inayokuzunguka,shirikiana na watu kwa hicho hicho kidogo ulichonacho.

“Being happy doesn’t mean that everything is perfect. It means you’ve decided to look beyond the imperfections.” –Unknown
Ahsante sana kwa kutembelea blog hii
Wako faraja mmasa a.k.a moa
Usikose kitabu changu pale kitakapotoka kitakachopatikana maeneo mengi

Share:

Story ya kusisimua:A Son’s Letter to His Mom









Sally jumped up as soon as she saw the surgeon come out of the operating room. She said: “How is my little boy? Is he going to be all right? When can I see him?”

The surgeon said, “I’m sorry. We did all we could, but your boy didn’t make it.”

Sally said, “Why do little children get cancer? Doesn’t God care any more? Where were you, God, when my son needed you?”The surgeon asked, “Would you like some time alone with your son? One of the nurses will be out in a few minutes, before he’s transported to the university.”Sally asked the nurse to stay with her while she said good-bye to son. She ran her fingers lovingly through his thick red curly hair.“Would you like a lock of his hair?” the nurse asked. Sally nodded yes. The nurse cut a lock of the boy’s hair, put it in a plastic bag and handed it to her . The mother said, “It was Jimmy’s idea to donate his body to the university for study. He said it might help somebody else. “I said no at first, but Jimmy said, ‘Mom, I won’t be using it after I die. Maybe it will help some other little boy spend one more day with his Mom.” She went on, “My Jimmy had a heart of gold. Always thinking of someone else. Always wanting to help others if he could.”

Share:

Teacher and Student Funny Conversation..



Teacher: Change this sentence into Future Tense, "I killed a person"
Student: The Future tense is "You will go to a jail"
Teacher: Did u make this poem yourself??
Student: Yes Sir !
Teacher: Nice to meet you, William Shakespeare
Teacher: Which one is more important for us, Son or Moon?
Student: Ofcourse Moon
Teacher: Why??
Students: The moon gives us light in night when we need it BUT the sun gives us light in day when we don't need it..
Teacher : What will you do after growing up?
Student : Facebooking
Teacher : No! I mean what will you Become?
Student : Admin of Facebook pages
Teacher : O My God! I Mean what will you Achieve when you grow up?
Student : Facebook Admin Rights
Teacher : Idiot! I Mean what will you do for you Parents ?
Student : I create a page for them on FacebooK."I Luv Mom and Dad".
Teacher : Stupid! What do you parents want from U? :@
Student : My Facebook password.
Teacher : Oh God
Share:

ZIFAHAMU FAIDA ZA KUFANYA MAZOEZI






Mazoezi ya viungo ni muhimu sana kwa afya yako, kuna namna mbalimbali za kufanya mazoezi. Unaweza kufanya mazoezi ya viungo fulani vya mwili wako kama miguu, mikono, mgongo nakadhalika. Lakini pia kuna mazoezi ambayo ukifanya utakuwa umefanya zoezi lilojumuisha kiungo zaidi ya kimoja mfano mazoezi ya kukimbia, kuruka kamba na mengineyo. Licha ya kuwa unaweza kutumia muda kidogo kufanya mazoezi kwa takribani dakika (30-45) kwa siku iwe asubuhi au jioni lakini pia unaweza kupata faida nyingi za kiafya kwa kufanya mazoezi hayo.

Kwakuwa kuna faida nyingi za kufanya mazoezi basi leo nimeona niorodheshe hizi chache kwa manufaa na ufahamu wa afya yako.
1. Mazoezi hukufanya uchangamke na kuwa shupavu.
2. Mazoezi huboresha ufahamu wako uwezo wa kuelewa na kufikiri mambo katika mazingira yanayokuzunguka.
3. Mazoezi huboresha uwezo wako wa kuhifadhi kumbukumbu.
4. Mazoezi husaidia kupunguza msongo wa mawazo.
5. Mazoezi huimarisha moyo hivyo hukuepusha na maradhi mengi yatokanayo na mapigo mabaya ya moyo.
6. Mazoezi humfanya mtu ajiamini.
7. Mazoezi hupasha mwili joto hivyo husaidia kuzuia baridi.
8. Mazoezi husaidia kuweka sawa kiwango cha cholesterol au mafuta yaliyopo mwilini.
9. Mazoezi hupunguza uwezekano wa mtu kupata ugonjwa wa kisukari.
10. Mazoezi hushusha kupanda kwa shinikizo la damu. (high blood pressure)
11. Mazoezi hupunguza uwezekano wa mtu kupata baadhi ya maradhi ya saratani.
12. Mazoezi humsaidia mtu kuondokana na baadhi ya matatizo ya akili.
13. Mazoezi huboresha hamu ya mtu kuweza kula.
14. Mazoezi hupunguza uzito wa ziada wa mwili na kufanya mwili wako kuwa mwepesi.
15. Mazoezi huimarisha mifupa hivyo hupunguza matatizo yatokanayo na kudhohofika kwa mifupa jina la kitaalamu (osteoporosis)
16. Mazoezi huboresha kinga ya mwili.
17. Mazoezi husaidia kuweka sawasawa mifumo mbalimbali ya mwili. Mfano: mfumo wa ufahamu, mzunguko wa damu, homoni na misuli.
Mpendwa msomaji hizi ni baadhi ya faida za kufanya mazoezi, yote ya yote mazoezi hurefusha maisha kwa kukufanya uwe mwenye afya njema. Ni vyema ukajiuliza, hivi ni kweli ukifanya mazoezi na kula vyakula bora kunaweza kuboresha maisha yako? Jibu ni NDIYO mazoezi na vyakula ni dawa pekee ya kutibu au kukuepusha na magonjwa mengi yanayoweza kuzuilika. Fanya mazoezi kuimarisha afya yako!

imeandikwa na saidi kamotta
ahsante kwa kutembelea blog hii
wako faraja mmasa a.k.a moa

usikose kitabu changu pale kitakapotoka


Share:

ZINGATIA MAMBO HAYA MUHIMU ILI KUWEZA KUBORESHA UHUSIANO NA MPENZI WAKO





Mara nyingi wengi wetu tumekuwa katika mahusiano na wapenzi wetu lakini hali sio kama ile ya awali wakati mnaanza mapenzi yenu.  Wanawake wengi wanalalamika kuwa  hawaoni upendo ule waliouzoea zamani wakati mapenzi yanaanza. Hata wanaume wengine wanalalamika pia kuwa penzi limeteremka kiwango baina yao.


Mara zote hushuka huku kwa ukaribu (intimacy) hakupangiliwi au kutazamiwa bali huja taratibu pasipo wapenzi kutambua, mara lugha hubadilika,  muda wakuwa pamoja hupungua, mambo huanza kufanywa kwa mazoea, vilivyo zoeleka kufanyika havionekani tena na taratibu hali hii ikikomaa huathiri hata tendo la ndoa. Katika hatua hii, wapenzi huanza kuchokana na kutotamaniana, hapa ndio kwenye upenyo wa mmoja au wote kuwaza njia mbadala.  Wengi walioachana au kutalikiana nao  walipitia njia hii pia.


Ili kuepuka yote haya, haunabudi kujifunza njia za kuwasha moto wa upendo kila wakati na kuongeza ukaribu (intimacy) kati yenu.


Njia za kukusaidia

1.       kucheka pamoja

Kicheko ni mlango wa ukaribu, kama mwaweza kucheka pamoja basi mwaweza kulia pamoja, na hapa mwaweza kuaminiana zaidi katika kuwasiliana hisia zenu, kama waweza kuitafuta furaha katika kila kitu basi unaweza kupenya katika vyote.  Usiwe mgumu na mwenye msimamo mkali katika kila kitu.  Jifunze kujizuia pale unapoanza kuelekea kwenye kukasirika na badala yake tumia kucheka kama mlango wa kutokea.  Kama utaanza kujizoeza  hivi ukiwa nyumbani, taratibu  utaweza ukiwa ofisini na hata kwingine kokote.
Share:

LISHE BORA YA MTOTO KUANZIA MIEZI 12-18





Kuanzia miezi 12 watoto wengi huwa wameanza kutembea na hivyo kuongeza michezo. Kutokana na kucheza zaidi watoto wanahitaji kula vizuri ili kuendeleza uzito na afya zao. Pia watoto wanakuwa wameota meno angalau nane hivyo wanaweza kutafuta chakula kilichopondwapondwa. Katika umri huu mtoto anaweza kula chakula chochote ambacho hana allergy nacho.

Ni vyema ukaandaa ratiba ya kumlisha mtoto wako na menu ya nini cha kumpa kila siku. Ratiba iwe mahali ambapo kila mtu anaweza kuiona kwa urahisi ili wote wanaohusika na malezi ya mtoto wajue nini mtoto anatakiwa kula na wakati gani. Kila siku hakikisha mtoto anapata vyakula kutoka kwenye makundi makuu ya vyakula; wanga, vitamini, protini na mafuta.


Vyakula kulingana na makundi haya ni kama ifuatavyo:

Wanga

         Nafaka
         Viazi
         Ndizi za kupika
Share:

KUHUSU MMILIKI WA BLOG HII

My photo
Naitwa faraja Mmasa a.k.a Moa,Mkazi na mzaliwa wa Wilaya ya Gairo Morogoro.KARIBU KATIKA BLOG hii tuelimishane mambo mbalimbali.Inatupasa kuwa na ufahamu wa mambo mbalimbali ili tuweze kuyatawala Mazingira yetu .Kuwa na Mwanasheria au Mhasibu haimanishi unatikiwa kujua au kufuatilia maswala ya uhasibu na sheria tu.Mfano nyumba yako au ndoa yako hutaindesha kwa taaluma uliyonayo.Vile vile huwezi kuendesha ujasiliamali kwa mafanikio kwa shahada yako ya uhandisi.TUNAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA

UJUMBE WA LEO

MIUJIZA MINGI INAYOTOKEA KATIKA MAISHA IPO KATIKA MAWAZO,FIKRA,NA IMANI ALIYONAYO MWANADAMU HUSIKA

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

GAR AD2

GAR AD2

GARI ADVERT

GARI ADVERT

Castrol

Castrol
Powered by Blogger.