Monday, April 28, 2014

MAMBO KUMI YA MSINGI YA KUFUATILIA UNAPOKUWA UNAJIANDAA NA MITIHANI



Habari za leo mfuatiliaji wa blog hii ya Faraja Mmasa Blog, natuamini ni mzima wa afya njema maana mungu wetu mpendwa anatupigania kila sekunde.Asante kwa kuwa mfuatiliaji wa mara kwa mara wa blog hii lakini pia nikupongeze kwa kuwa mfuatiaji wa mara kwa mara kwa kuwa kila unapoingia katika blog hii basi kuna kitu kipya unajifunza kila siku katikachokusaidia katika maisha yako ya  kila siku.Mada  ninayotaka kuilezea leo inahusu hasa wanafunzi wa kidato cha sita wanaokwenda kujiandaa na mitihani yao ya kumaliza kidato cha sita,Mimi ninawaombea sana kwa mwenyezi mungu kila mmoja akafanye mitihani kwa utulivu na kuweza kusonga mbele, nimeinadika mada hii kwa ajili ya wanafunzi wote wa kidato cha sita lakini pia na mimi pia mdogo wangu kipenzi wa mwisho Jackline Kaboko anajiandaa kufanya mtihani huo,kwa hio nikaona sio vyema kukaa na kumuelezea nini cha kufanya peke yake basi ,bali niongee na wanafunzi wote wanaojiandaa na mtihani huu.Mada hii pia nitaifundisha katika Redio ya Sibuka 94.5 fm siku ya jumatatu na alhamisi kuanzia  saa tisa na dakika 20,hivyo basi pia unaweza kunisikiliza kupitia Radio.
Swala la maandalizi kwa mwanafunzi katika kipindi hichi cha mwisho ni kitu muhimu zaidi ingawa kuna msemo umejijenga katika vichwa vya watu wengi “NG’OMBE HANENEPI SIKU YA MNADA” ndugu mwanafunzi kataa kabisa usemi huu kuuweka katika kichwa chako, hata mimi nilipokuwa mwanafunzi nilikataa kabisa msemo huu,mimi nilikuwa naamini kuwa “NG’OMBE ANANONA SIKU YA MNADA” (angalizo lakini sio kusoma kitu kipya mpaka dakika ya mwisho unaingia  kwenye chumba cha mtihani) na wewe pia amini ng’ombe ananona siku ya mnada.Hakuna kitu muhimu kama siku za mwisho za kujiandaa na mitihani yako,unaweza ukawa umejiandaa vizuri sana huko nyuma lakini kipindi kiki cha mwisho ukamaliza vibaya na kukupelekea kushindwa kufanya vizuri katika mitihani yako.Kipindi hichi cha mwisho ni kipindi cha utulivu, lakini pia nakuomba kama kuna mzazi au mlezi anasoma mda hii basi nomba wewe ndio uwe chanzo cha kufanya mwanao anapata utulivu,acha kumgombeza ovyo mtoto katika kipindi hichi na kumsema maneno makali ya kumfanya kukosa ule utulivu wa ndani,pia kama mwanao anakaa nyumbani hakai shuleni basi pia katika kipindi hichi naomba umtoe katika ratiba za kazi za nyumbani,mpe muda wa kutosha sio mtoto anarudi nyumbani basi jambo la kwanza kumwambia kuna vyombo vya kuosha vinakusibiri! Wiki hii mpe likizo mwache asome zaidi na apate muda wa kupumzika wa kutosha.Mambo kumi ya kufuatilia katika kipindi hichi ni kama yafuatayo;
1.      KUWA MTU WA SALA AU KUWA KARIBU NA MWENYEZI MUNGU.
Kwa mwanadamu wowote yule ni jambo la lazima kuwa mtu wa sala muda wote  ingawa maisha ya kudunia yanatusonga na kutufanya kumsahamu mwenyezi mungu na kuyashika ya dunia.Mwanafunzi hata kama umekuwa nyuma sana katika maswala ya kiimani basi hichi ndio kipindi cha kuwa karibu na mungu wako,ongea na mungu ,omba sana ,mwombe mungu akupe wepesi katika mitihani yako,mwombe mungu akulinde na yote mabaya yanayoambatana katika kipindi hichi cha mtihani maana ndicho kipindi amabcho kwa wanafuzi huwa yanazuka magonjwa na haijulikani yametokea wapi ,hayo magonjwa mara kichwa kinagonga,mara sioni vizuri basi ni kipindi cha kupigana na nguvu za  giza,mwombe mungu akuepushe na watu wabaya wanaotaka kuinuka katika kipindi hichi,omba utulivu,ule utulivu wa kutoka ndani,omba kumbukumbu yako vizuri ,ushindwe hali ya hofu,pia usijinee mabaya katika kipindi hichi,lia na mungu wako maana elimu yako ndio maisha yako,mkabidhi mungu kila kitu,pia kama ni mkristo basi pia mshirikishe kiongozi wako wa kiroho akuweke kwenye maombi au kama muislamu basi pia muone sheikh au ustadhi au kiongozi wowote yule mfanye dua na sala. Mwambie mungu nishike katika kipindi hichi.
2.      TUMAINI LA KUFAULU KUWA KUBWA KULIKO  HOFU YA KUSHINDWA.
Hili ni jambo la msingi zaidi na kulitilia maanani kwa mwanafunzi  hasa katika kipindi hichi anachojiandaa na mitihani yake,hili pia linachangia kwa kiasi kikubwa  “NG’OMBE KUNENEPA SIKU YA MNADA”. Hakuna kitu kibaya kwa mwanadamu kama hofu tena hofu mbaya zaidi ni FEAR OF FAILURE .Hofu ya kushindwa ni tatizo kubwa kwa mwanadamu kuweza kufika malengo yake,wanafuzni wengi wanashindwa mtihani hata kabla hawajaingia katika chumba cha mtihani,wengi wao wanakuwa tayari wameshashindwa,mwanafunzi anakuwa tayari  ameshashindwa kutokana na hofu ,anajipima uwezo wake wake yeye mwenyewe na kujiona hawezi tena ,unakuta ni kipindi ambacho mwanafuzni anakumbuka mitihani yote aliyoshindwa  siku za nyuma na kujiona hawezi tena ,tena unakuta anajisemea moyoni “hii mitihani ya kawaida imenishinda ije kuwa huu wa taifa?” lakini kumbuka ujianavyo moyoni mwako ndivyo ulivyo vile vile hakuna kitu kibaya na kizuri kama ulimu wako ,ulimi unalaani lakini pia ulimi unabariki,.katika kipindi hichi chakujiandaa wacha kinywa chako kijae ushindi ,jione umeshashinda na sasa unasubiri muda tu wa kuingia kwenye chumba cha mtihani,kumbuka mitihani yote uliyofanya vizuri ,kumbuka 90 zote ulizopata na jisimee mwenyewe kimomoyo ninakwenda kushinda sasa na kusonga mbele,ni wakati wangu wa kuingia elimu ya chuon kikuu,kuna habari moja nilisoma katika kitabu cha “THINK AND GROW RICH” kama hujawahi kusoma hichi kitabu kitafute kitakubadilisha fikra na mitazamo ya maisha ndani ya saa moja tuu ,kama huamini kisome utakuja kunipa majibu. Habari hio iilikuwa inamhusu mkuu wa jeshi  ambaye alikuwa anaongoza jeshi kwenda vitani  basi alichokifanya mkuu huyo wa jeshi walipokwenda kwenye uwanja wa mapigano walitumia usafiri wa kwenye maji walitumia boti za kivita,walipofika kwenye uwanja wa mapambano mkuu yule majeshi akaamrisha boti zote “ZICHOMWE MOTO”  wanajeshi wake wakamshangaa lakini hawakuwa na jinsi zaidi ya kukubari amri,walivyomaliza akawaita wanajeshi wake na kuwaambia sasa tumekuja kupambana na ni LAZIMA TUSHINDE ILI TUWEZE KURUDI NYUMBANI maana hatuna vyombo vya kusafiria kutuwezesha kurudi nyumbani kwa hiyo lazima tushinde ili  tuchukue vyombo vyao turudi nyumbani,hio kitu kikawaingia wanajeshi akilini wakajua njia ya kurudi nyumbani kuungana na familia zao tena ni KUSHIND TU hivyo wakapigana kwa akili na nguvu zao zote mwishoni WAKASHINDA! Hivyo hivyo mwanafunzi wa kidato cha sita jisemee moyoni na iweke akilini  mwako “NI LAZIMA NIFAULU KWA NJIA YOYOTE ILE NA KUJIUNGA ELIMU YA CHUO KIKUU”.Jinenee ushindi mdogo wangu usiogope amini uwezo unao na umejiandaa vya kutosha  kiasi cha kwenda kufaulu.
3.      SIO KIPINDI CHA KUJIFUNGIA NDANI PEKE YAKO NA KUKESHA
Katika kipindi hichi cha mwisho cha kujiandaa na mitihani yako si kipindi cha kujifungia ndani peke yako na kujisomea ndani ,hichi ni pindi cha kujichanganya na wenzio tena wa shule mbalimbali mi wakati nasoma Advance nilikuwa na camp mbalimbali za kujisomea ambazo tulikuwa tunakutana shule zaidi ya kumi,mdogo wangu acha kujifungia ndani hii dunia tuliyonayo ni dunia ya taarifa,jichanganye na wenzio fanya sana group discusion ujue mambo usiyoyajua na mapungufu uliyonayo na kipi upo vizuri,hakuna njia rahisi ya kusoma na kukumbuka kitu kama kusoma kwa makundi hii itakuwezesha hata unapokuwa katika chumba cha mitihani kukumbuka kwa urahisi tena utakumbuka hata aliyetaja hio pointi wakati mpo kwenye discussion. Hata siku moja usiamini unajua kila kitu,jua kabisa kuna vitu unahitaji kupata kutoka kwa wengine ,kama baadhi ya vitu hujui wenzio wanajua ,pia kuna watu wengien ni mabingwa wa kuotea maswali,akisema hili lipo jua basi kweli utalikuta,mimi wakati nasoma nilikuwa na rafiki yangu anaitwa Benedict Baraka Stambuli huyu nilikuwa namwania sana katika utabiri wa maswali na kweli nilikuwa nayakuta hivyo basi kabla ya mtihani lazima nilikuwa nimtafute naamuliza eeh mtaalamu wangu vipi leo maswali yapi yanakuja?.Lakini pia katika kipindi hiki cha mitihani huwezi jua bwana kama unavyojua kwenye wengi kuna mengi nadhani umenielewa ninachomaanisha sio lazima niseme kila kitu.
4.      YAJUE MAENEO MUHIMU NA KUWEKA NGUVU KUBWA
Hili pia ni jambo la msingi kujua wapi unatakiwa kuweka nguvu katika kipindi cha mwisho cha kujiandaa na mitihani yako ya mwisho ,katika kuweka nguvu unatakiwa kuweka mkazo katika mambo mawili
a)      Yale msaomo ambayo unahakika unayajua vizuri na uelewa mkubwa
Mara nyingi kila mwanafunzi anakuwa na masomo ambayo anajua anafanya vizuri hivyo basi ni vizuri kuweka nguvu kubwa katika hayo masomo maana ndio yatanyanyua Division yako ,hakikisha masomo ambayo unauwezo  nayo wa kufaulu hukosi chini ya B+ .Hakikisha unakufa nayo ,jua hayo ndio mkombozi wako,lakini kumbuka pia unatakiwa kuweka nguvu pia kwenye masomo mengine pia maana usije pata A huku kwingine unapata F jua utashusha division yako maana matokeo yote huwa yanatafutwa kwa kwa kanuni ya LAW OF AVERAGE
b)      Uliko na mapungufu na kuna maksi nyingi
 Lakini pia lazima uweke nguvu kubwa kwenye sehemu yenye mapungufu ambayo unajua maswali yake yana maksi nyingi. Kipindi hichi cha mwisho lazima ujue ni eneo gani una mapungufu lakini nieneo ambalo linaulizwa sana kwenye mitihani ,hapa sasa ndio umuhimu wa kujua umuhimu wa kujua mfumo wa mtihani unavyokuja nitalielezea hili kwenye point inayokuja.Ukishajua mapungufu uliyonayo na wewe mwenyewe huwezi basi mtafute mwalimu au mwanafunzi mwenye uwezo nalo akupe msaada.
5.      KURUDIA ZAIDI MITIHANI ILIYOPITA NA KUUJUA MUUNDO WA MITIHANI ILIVYO.
Katika hichi kipindi cha mwisho cha kujiandaa na mtihani  hasa katika mwezi wa mwisho ni vizuri zaidi mwanafunzi kupitia mitihani ya nyuma ya kutosha kuna material mengi yameandaliwa yenye mitihani toka ya mwaka 1980 au kuna vitabu vyenye maswali na majibu ya mitihani ya taifa toka miaka ya nyuma,kwa hiyo ni vizuri kupitia mitihani ya kutosha ili kujiweka fiti,kujua mitihani inakuja vipi na inajibiwa vipi hata kama watarudia maswali basi itakuwa faida kwako kama uliyapitia maana kufanya swali unalolijua tayari lina faida nyingi ndani ya chumba cha mtihani,kwanza itakuwezesha kupata maksi nyingi lakini pia itakuwezesha kutumia muda mdogo na hivyo kutumia muda mwingi kwenye maswali mengine hivyo kuongeza kiwango chako cha kufaulu.Lakini pia kama upo na rafiki yako mnaweza kujipima kwa kuchagua mtihani mmoja ,mwishoni mkabadilishana mkasahishiana kwa kuangalia majibu au mkapelekea mwalimu mkamwomba naamini atawasaidia.Laini pia ni muhimu kuangalia mtaala katika upande wa mitihani maana huwa mwanatoa mtihani mzima utakavyokuwa na kila kipingele kitakuwa na maswali kutoka topic gani.
6.      HAKIKISHA PIA UNAPATA MUDA WA KUTOSHA WA KUPUMZIKA NA KULALA.
Katika kipindi hichi cha mwisho ndio baadhi ya Wanafunzi hugeuka kuwa NDEGE WAKATI WAO NI BINADAMU, hapa wanafuzi hugeuka kuwa bundi maana bundi tu ndio huwa anakesha usiku.Najua hichi ni kipindi cha kusoma sana lakini pia ni lazima ujipe muda wa kutosha wa kupumzika ili uweze kuutendea haki ubongo,unajua  uwezo wa mwanadamu wa kuelewa una masaa na ukizidisha hapo basi unakuwa huingizi tena ,unakuwa unasoma maandishi kama picha,lakini pia hakuna kitu muhimu  kama kulala muda wa kutosha,usipo lala muda wa kutosha unasababisha matatizo mengine kama msongo wa mawazo,uwezo mdogo wa kufikiri na kijifunza,ufanisi kuwa mdogo ,hivyo basi ni lazima uhakikishe unapata muda wa kupumzika na kulala katika hichi kipindi cha kujiandaa na mitihani,usigeuke kuwa ndege wakati wewe ni mwanadamu maana unaweza kuna msemo unasema MSULI TEMBO MATOKEO SISIMIZI. Wakati mwingiine unatakiwa uusikilize mwili , kama mwili na akili vimechoka pumzika ,hakuna ubingwa wa kukesha,na wakati umelala ni vizuri hakikisha kama una simu umezima ili kuepuka usumbufu wa kuamshwa wakati simu inaita au toa sauti ukiamka utazikuta missed call lakini pia wape taarifa watu waliopo karibu hutaki kuamshwa mpaka muda wako wa kuamka utakapofika wa kuamka ili uweze kupata usingizi mzuri  ukiamka unakuwa kiumbe kipya chenye nguvu mpya.
7.      HAKIKISHA UNAKUWA NA MATERIAL NA NOTES NZURI AU NONDO ZILIZOSHIBA.
Pia kwa mwanafunzi hakikisha  unakuwa na malighafi nzuri,kama ilivyo kiwandani ili uzalishe bidhaa yenye ubora ni lazima malighafi nzuri,hivyo basi kwa mwanafunzi unatakiwa kuwa na material mazuri ya kushiba katika kipindi hicho cha mwisho,kusanya material kwa wanafunzi wanaofanya vizuri unaowajua pia tafuta material katika zile shule zinazofanya vizuri kama st fransics,mzumbe,,feza boys marian girls. Inakuwaje unaona material kutoka shule nzuri inayofanya vizuri unaliacha tu linapita kirahisi rahis tu? Unaweza kusoma sana lakini ukasoma vitu sio sahihi baadae matokeo yakawa tofauti na msuli uliopiga,sisi mwanzoni tuliosoma shule za KAYUMBA tunalijua hili,asilimia kubwa ya wanaofeli pia ni kutokuwa na material sahihi,lakini pia hakikisha unapata yaliondikwa kwa lugha unayoielewa,maana waandishi wengine wanataka sifa kwa kufanya mambo kuwa  magumu.
8.      HAKIKISHA UNAHUDHULIA  SHULENI NAKUSIKILIZA MAELEZO YA MWISHO YA WALIMU.
Katika kipindi hichi cha mwisho pia imekuwa ni jambo la kawaida kwawanafunzi wengi kutopenda kuhudhuria shuleni na kujifungia wanapokujuawao,lakini hichi ni kipindi kizuri pia kuhudhuria shuleni na kujua maelezo yoyote mtakayopewa lakini pia mwanafunzi asidharau mwalimu anaposema ana kitu cha mwisho anataka kufundisha ,huwezi jua kwanini mwalimu anataka kufundisha kipindi hicho,hivyo ni vizuri kwenda kusikilizana kujiona umetimilika,unaweza ukashangaa peke yakounasema mwalimu mbona hichi akufundisha lakini kila mtu akakushaangaa maana mwalimu alishakifundisha mwishoni,mara nyingi haya mambo huwa yanatokea.

9.      HAKIKISHA KUMBUKUMBU ZAKO ZINAONGEZEKA KADRI JINSI MUDA UNAVYOZIDI KWENDA.
Katika kipindi hichi cha mwisho mwanafunzi hakikisha kumbukumbu za vitu vyote ulivyosoma unaongezeka jinsi muda unavyozidi kwenda na kukaribia kufanya mitihani,maana kwenye mitihani unaingia wewe kama wewe,hakikisha unapata muda peke yako mtulivu kusikokuwa nakelele ya aina yoyote unaanza kuangaliamaswali unaanza kujijibu wewe mwenyewe kama vile kuna mtu anakuuliza au unawezakuwa unaandika kamani pointi unaandikakwenye karatasi,hii itakuwezesha kujua wapi kuna mapungufu hivyo kutilia mkazo zaidi katika hilo eneo ambalo unaona bado haupo sawa.
10.  KUANDAA SUMMARY KATIKA MASOMO YAKO
Hichi kipindi cha mwisho pia,ni kipindi cha kujiandalia summary za notes zako za kwenye madaftari na vitabu maana itafika mwisho wa siku utashindwa kusoma madaftari na vitabu vyote,hivyo basi yale mambo ya msingi yote yaweke kwenye summary hii itakuwezesha kurudia mambo mengi kwa muda mdogo,na hivi vitu utaweza kuvikumbuka kwa urahisi zaidi.
Asante kwa kufuatilia somohili lakini pia usikose sehemu ya pili ya somo hili siku ya alhamisi nitaelezea  MAMBO YA MSINGI YA KUFANYA KABLA YAKUINGIA CHUMBA CHA MTIHANI WAKATI UPO NDANI YA CHUMBA CHA MTIHANI NA BAADA YA KUTOKA CHUMBA CHA MTIHANI
Kama wewe ni mwanafunzi na una hofu sana katika kipindi hichi cha kujandaa mwishoni au ni mzazi unataka ushauri kwa ajili ya mwanao basi unaweza kunipigia kwenye namba 0658494977.
Wako Faraja Mmasa a.k.a MOA
X+3P’S
*SELF FULFILLING PROPHECY*

****Tafuta mafanikio kama utaishi milele lakini kumbuka kutenda mema nakumcha mungu kamaleo ndio siku yako ya mwisho kuwepo katika dunia hii*******
Share:

2 comments:

KUHUSU MMILIKI WA BLOG HII

My photo
Naitwa faraja Mmasa a.k.a Moa,Mkazi na mzaliwa wa Wilaya ya Gairo Morogoro.KARIBU KATIKA BLOG hii tuelimishane mambo mbalimbali.Inatupasa kuwa na ufahamu wa mambo mbalimbali ili tuweze kuyatawala Mazingira yetu .Kuwa na Mwanasheria au Mhasibu haimanishi unatikiwa kujua au kufuatilia maswala ya uhasibu na sheria tu.Mfano nyumba yako au ndoa yako hutaindesha kwa taaluma uliyonayo.Vile vile huwezi kuendesha ujasiliamali kwa mafanikio kwa shahada yako ya uhandisi.TUNAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA

UJUMBE WA LEO

MIUJIZA MINGI INAYOTOKEA KATIKA MAISHA IPO KATIKA MAWAZO,FIKRA,NA IMANI ALIYONAYO MWANADAMU HUSIKA

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

GAR AD2

GAR AD2

GARI ADVERT

GARI ADVERT

Castrol

Castrol
Powered by Blogger.