Thursday, May 1, 2014

MBINU ZA KUONGEZA MAUZO KATIKA BIASHARA YAKO.


Karibu katika blog hii ,natumaini u mzima wa afya njema maana mungu  wetu anaendelea kutupigania.Leo nilitaka kuongelea mada hii ya kuongeza mauzo katika biashara,kama tunavyojua moyo wa biashara ni mauzo,kama hakuna mauzo basi hakuna biashara.Kabla sijaanza kulielezea zaidi mada hii kama ndio mara yako ya kwanza kusoma blog hii,basi pia mwenye blog hii pia ni mshauri katika mambo ya biashara ,pia katika maswala ya saikolojia na Afya ,kama unatatizo lolote basi unaweza kupiga simu au kutuma msg katika namba 0658494977 kwa ushauri zaidi.
Kama nilivyosema hapo mwanzo Mauzo ndio moyo wa biashara,kama hakuna mauzo hakuna biashara,kama ilivyo kwa mwanadamu bila Moyo hakuna Uhai ,hivyo hivyo kwenye biashara kama hakuna Mauzo basi hakuna Biashara,basi ni lazima kwa mfanyabiashara yoyote yule mara zote kusumbua akili yake namna gani anaweza kuongeza mauzo katika biashara yake,leo nitaongelea mambo ya msingi matatu katika kukuza mauzo katika biashara yako



1.     ONGEZA IDADI YA WATEJA KILA SIKU.
Kama mfanyabishara huna budi kuongeza idadi ya wateja kila siku kama unataka kuongeza mauzo katika biashara yako. Hasa kama unafanya biashara ya bidhaa ambazo mtu hanunui kila siku basi inakupasa kuongeza idadi ya wateja,kuna bidhaa nyingine mtu akinunua mara moja basi anaweza tena asinunue tena  katika maisha yake au anunue tena baada ya mwaka mpaka  mwaka ,kama wanao fanya biashara za magari,battery za magari,funitures na biashara yoyote ile ambayo mtu hafanyi manunuzi ya mara kwa mara, hivyo basi kwa biashara kama hii,njia sahihi ya kukuza mauzo yako hakikisha unaongeza wateja kila siku,wingi wa wateja ndio wingi wa mauzo yako,hakikisha unakuwa  na kumbukumbu za wateja wako,hivyo basi wingi wa wateja ndio wingi wa mauzo.

2.     HAKIKISHA UNAUZA IDADI KUBWA YA BIDHAA KWA KILA MTEJA.
Njia nyingine ya kuongeza mauzo katika biashara yako basi hakikisha kila mteja anayenunua kwako,ananunua bidhaa nyingi zaidi,katika swala la huduma kwa wateja,mteja anapokuamini mpaka kufanya biashara na wewe basi yupo tayari kukusikiliza,hivyo basi hakikisha mteja hata anapotaka kununua bidhaa moja basi hakikisha una mshawishi kununua kwa wingi kutoka kwako,lakini vile vile kuna bidhaa ambazo zinatumiwa kwa pamoja,hivyo basi akichua bidhaa moja unaweza kumwambia ungechukua na hii itakuwa vizuri zaidi au kama ni unawauzia wafanyabiashara wanaoenda kuuza jumla basi unaweza kumtengenezea wewe manunuzi yake,pia unaweza kumpa mteja discount au bonus akinunua kitu kingine kwa wakati huo,hii pesa utakayopata itakuwa ni ziada kwasababu usingeipata kama mteja asingenunua kitu cha ziada.Njia hii mara nyingi unategemea na mpango mkakati ulio nao,au kama kwako ni ngumu basi nipigie 0658494977 kwa ushauri zaidi.
3.     HAKIKISHA MTEJA ANANUNUA MARA NYINGI AU MARA KWA MARA
Hii pia ni njia bora zaidi ya kuongeza mauzo katika biashara yako. Kama unauza bidhaa ambazo mteja anatumia mara kwa mara kama vile vyakula,vinywaji(soda,juice) n.k unatakiwa  uhakikishe mteja anunue mara kwa mara kutoka kwako .Njia ya kumfanya mteja kwako  kununua mara kwa mara ni kuhakikisha anapata kitu cha ziada kutoka kwako lakini wewe haikugharimu chochote  na hii unaweza kufanya labda kwa kutoa huduma nzuri kwa wateja,mteja akajiona nathamni kubwa na hivyo hivyo kutaka kununua mara nyingi kutoka kwako,unaweza kuwatumia msg wateja wako kila wanapofanya manunuzi kutoka kwako,kuwaambia ahsante au mara nyingine unaweza kuwapigia simu kuwajulia hali,au kama mteja  hujamwona siku nyingi basi unaweza kumpigia simu kumjulia kulikoni maana hujamwona siku nyingi,hii itamfanya mteja kukuona wewe kama ndugu yake na hivyo hatawaza kwenda kununua kwa mtu mwingine.
Ndugu msomaji wa blog hii fahamu kumpata mteja mpya ni ngumu zaidi kuliko kumbakiza mteja wako wa siku zote,hivyo hakikisha mteja uliye naye tayari haondoki au haachi kufanya biashara na wewe.

Kwa ushauri zaidi wa kibiashara au kama una mtaji mdogo hujui biashara gani ufanye piga namba 0658494977
WAKO FARAJA MMASA A.K.A MOA
*SELF FULFILLING PROPHECY*

X+3P’S
Share:

0 comments:

Post a Comment

KUHUSU MMILIKI WA BLOG HII

My photo
Naitwa faraja Mmasa a.k.a Moa,Mkazi na mzaliwa wa Wilaya ya Gairo Morogoro.KARIBU KATIKA BLOG hii tuelimishane mambo mbalimbali.Inatupasa kuwa na ufahamu wa mambo mbalimbali ili tuweze kuyatawala Mazingira yetu .Kuwa na Mwanasheria au Mhasibu haimanishi unatikiwa kujua au kufuatilia maswala ya uhasibu na sheria tu.Mfano nyumba yako au ndoa yako hutaindesha kwa taaluma uliyonayo.Vile vile huwezi kuendesha ujasiliamali kwa mafanikio kwa shahada yako ya uhandisi.TUNAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA

UJUMBE WA LEO

MIUJIZA MINGI INAYOTOKEA KATIKA MAISHA IPO KATIKA MAWAZO,FIKRA,NA IMANI ALIYONAYO MWANADAMU HUSIKA

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

GAR AD2

GAR AD2

GARI ADVERT

GARI ADVERT

Castrol

Castrol
Powered by Blogger.