Wednesday, May 7, 2014

NAMNA YA KUANDIKA MCHANGANUO WA BIASHARA

                      

Mpango wa biashara unasaida kufanya uamuzi mbalimbali kusuhusu mwenendo mzima wa biashara, kupima mwelekeo na ukuaji wa biashara.

Mchanganuo wa biashara ni andiko linalofafanua namna biashara inavyoweza kuanzishwa au kuendelezwa. Kitaalam, unatakiwa uwe na mpango wa biashara kabla ya kuanza biashara yoyote.

Mpango wa biashara unasaida kufanya uamuzi mbalimbali kusuhusu mwenendo mzima wa biashara, kupima mwelekeo na ukuaji wa biashara.

Pia mwenendo wa biashara unasadia  ugundua mapungufu katika uendeshaji biashara na kubaini fursa za kupanua biashara. Ufuatayo ni mtririko wa mchanganuo wa biashara.

Jalada la nje: Linahusisha jina la biashara, muda wa mpango (mfano. 2013 – 2015), anuani ya biashara, toleo, jina la aliyeandaa, mwaka pamoja na kuonyesha mchanganuo unaelekezwa kwa nani.

                                                        DIBAJI

Sehemu hii huandikwa muhtasri wa mambo mbalimbali yaliyoanishwa katika mchanganuo mathalani, aina ya biashara, bidhaa au huduma zinazotolewa kwa ufupi, mpango wa mauzo, mpango wa ukuaji kwa mwaka, soko lengwa, mtaji unaohitajika, namna mwekezaji au mdau anavyoweza kunufaika iwapo akiwekeza au benki ikikupatia mkopo namna gani utalipa.

                                                 
                                   MAELEZO YA BIASHARA

Dira/ndoto, madhumuni, historia fupi ya biashara, bidhaa au huduma inayotolewa kwa mapana, uchanganuzi wa hali ya tasnia kwa sasa na siku zijazo, uchanganuzi wa hali ya biashara kwa kuainisha upungufu na nguvu ndani ya biashara, fursa na vihatarishi katika mazingira yanayoizunguka biashara.

                                                         
                                             MASOKO
inazungumzia hali ya soko katika tasnia ya biashara husika, soko unalopanga kuuzia bidhaa au huduma, unaweza kuchukua nafasi gani katika soko hilo kwa asilimia.

Mbinu unazotumia kufikisha bidhaa au huduma kwenye soko, mpango wa mauzo kwa mwezi, kwa mwaka hadi muda wa mpango uliojiwekea mathalani miaka 3 mpaka 5, mpango wa bei, hali ya ushindani, mbinu za kuendana na ushindani katika soko, namna ya kutangaza biashara, na unapaswa kuangalia ni jinsi gani utaweka kipaumbele katika kutangaza bidhaa kama una zaidi ya bidhaa moja.

                                                 
                                  MENEJIMENTI NA UTAWALA
Menejimenti na utawala: Mfumo wa biashara kama ni ya mtu mmoja, ubia au kampuni, chora chati ya mtiririko wa madaraka, wasifu wa maofisa wa ngazi za juu mathalani Mkurugenzi Mtendaji na wakurugenzi wengine, idadi ya wafanyakazi kwa sasa, mpango wa ukuaji au kuongezeka kwa wafanyakazi, mfumo wa umiliki kama ni kampuni-weka mchanganuo wa hisa za kila mmliki, kama ni ubia elezea mchango wa kila mmoja na namna ya kugawana maslahi, toa mchanganuo kwa wataalam mbalimbali unaowatumia katika biashara mathalani mshauri wa biashara, mwanasheria, wasafirishaji, na wakaguzi.

                                                         
                                            MAMBO YA FEDHA
Weka makisio ya mizania, mapato na matumizi na mtiririko wa fedha kwa muda wa mpango tangu sasa.

Maelezo ya dhana ya kifedha iliyotumika kupanga makisio, muundo wa mtaji (ainisha kiasi cha mtaji binafsi, msaada, mikopo, na njia nyinginezo kama zipo).

Mwisho ni mpango wa kupata fedha kama zinatoka kwa wawekezaji au benki- kiasi gani unahitaji kwa muda gani na namna gani utalipa kwa faida gani.
Mchanganuo wa vihatarishi vya biashara: Ainisha vihatarishi vya biashara yako, fursa za kibiashara zinazoendena na vihatarishi hivyo, mchanganuo wa itakuwaje endapo mipango uliyojiwekea haitatekelezeka, mchanganuo vihisishi, kwa mfano namna gani bei ikipanda au kushuka inaweza kubadilisha mwelekeo wa biashara yako.
    


           RATIBA ZA UZALISHAJI BIDHAA AU UTOAJI  HUDUMA
 Mara nyingi  ratiba ya uzalishaji inafanywa kwa programu za kinakilishi.
Viambatanisho: Viambatanisho mbalimbali huwekwa kulingana na mtumiaji wa mchangunuo huo mathalani wasifu binafsi wa maofisa wa ngazi za juu, nakala ya vyeti vya usajili, TIN, VRN, leseni na vibali vya biashara.
Kwa mjasiriamali ni vizuri  kujua yaliyomo katika mchanganuo wa biashara kwa sababu utakusaidia  kuelezea biashara yako kwa ufasaha sehemu yoyote. Haijalishi hata kama huwezi kuandaa mchanganuo, lakini kujua mambo ya msingi ni jambo la busara sana.

Wajasiriamali wengi wamekuwa wakikosa mikopo benki kutokana na kuandaliwa mchanganuo mbovu, kumbe hata kabla hujapeka ni vizuri wewe ujiridhishe kwa taarifa zilizomo.

Kama unataka kuandikiwa mchanganuo mzuri wa mpango wa biashara (Business Plan) kwa ajili ya kuomba mkopo  katika taasisisi za fedha Benki,Saccos n.k piga namba 0658494977

WAKO FARAJA MMASA A.K.A MOA
*SELF FULFILLING PROPHECY*

X+3P’S
Share:

0 comments:

Post a Comment

KUHUSU MMILIKI WA BLOG HII

My photo
Naitwa faraja Mmasa a.k.a Moa,Mkazi na mzaliwa wa Wilaya ya Gairo Morogoro.KARIBU KATIKA BLOG hii tuelimishane mambo mbalimbali.Inatupasa kuwa na ufahamu wa mambo mbalimbali ili tuweze kuyatawala Mazingira yetu .Kuwa na Mwanasheria au Mhasibu haimanishi unatikiwa kujua au kufuatilia maswala ya uhasibu na sheria tu.Mfano nyumba yako au ndoa yako hutaindesha kwa taaluma uliyonayo.Vile vile huwezi kuendesha ujasiliamali kwa mafanikio kwa shahada yako ya uhandisi.TUNAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA

UJUMBE WA LEO

MIUJIZA MINGI INAYOTOKEA KATIKA MAISHA IPO KATIKA MAWAZO,FIKRA,NA IMANI ALIYONAYO MWANADAMU HUSIKA

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

GAR AD2

GAR AD2

GARI ADVERT

GARI ADVERT

Castrol

Castrol
Powered by Blogger.