Tuesday, February 25, 2014

HISA-1



Habari za leo unayesoma blog hii,natumainI wewe ni mzima wa afya njema,mungu anazidi kukupigania kila siku.Nimekuwa siku nyingi  nikihaidi kutoa elimu kuhusu hisa ,leo basi naanza kuelezea kwa undani kuhusu somo la HISA.Naamini mpaka mwisho wa somo hili utakuwa umepata ujasiri wa kuwekeza kwenye SOKO LA HISA,mimi nimeanza kidogo sasa ,lengo langu baada ya miaka kumi niwe nimewekeza kwa kiwango kikubwa na kuchuma faida kubwa.



Hisa ni mali.Hisa ni rasilimali.Hisa ni kitega uchumi kinachoweza kukupa fedha.Hisa ni hatimiliki ya kampuni.Hisa ni biashara.Hisa hukuwezesha kupata fedha kupitia mikopo,Hisa hukufanya kupata nguvu ya maamuzi.Hisa ni mtaji.kumiliki UCHUMI na FAIDA kupitia makampuni,hutegemea umiliki wa hisa.HISA SIYO KIPANDE CHA MSINGI BALI NI HAZINA.


Hisa ni kumiliki kampuni,ukitaka kumiliki kampuni ,nunua na umiliki hisa zake,kama vile hati ya kumiliki ardhi (title deed) inavyoonyesha ushahidi wa kumiliki ardhi ;kadhalika cheti cha hisa ( share certificate) kinathibitisha umiliki wa kampuni wa biashara.Kiwango cha umiliki wa kampuni  hutegemea idadi ya hisa  anazomiliki mwanahisa.kumiliki hisa ni kuwekeza kwenye kampuni,kama unamiliki hisa nyingi,zaidi ya asilimia 50%,basi unakuwa na nafasi kubwa ya kufanya uamuzi katika kampuni inayohusika.


Kampuni inaweza kupata kama mtaji wa kununua rasilimali,mitambo,mashine,kuendesha biashara na kwa kuuuza hisa zake,hivyo hisa zinazouzwa zinaleta fedha kwa kampuni kama mtaji wa biashara.Ukinunua hisa unatoa fedha na ukiuza hisa unapata fedha. Hisa  humpatia mwanahisa faida kwa njia ya gawio,ongezeko la thamani,mkopo na kadhalika,nitaelezea zaidi mada za mbele. Kama kampuni ina mtaji wa shilingi laki moja na wewe umenunua hisa za shilingi elfu hamsini, maana yake utakuwa na nguvu ya kushiriki hata kwenye maamuzi nyeti yahusuyo kampuni au biashara husika, tofauti na mtu mwenye hisa za kwa mfano shilini elfu kumi.


Mtu akisema nina hisa NMB anamaanisha ana miliki NMB. Umiliki huu unajionyesha wazi na bayana wakati wa kufanya maamuzi na kugawana gawio (faida inayopatikana katika kampuni). Mwenye hisa nyingi huwa na sauti au ushawishi mkubwa katika kufanya maamuzi na hupewa gawio kubwa kwa uwiano wa hisa zake.
Hisa ni mali iliyorahisi kubadilishwa na kuwa fedha taslimu kama vile ardhi,nyumba,mitambo na mashine ni mali kwa kuwa zina thamani,hisa ni rahisi zaidi kuibadilisha na kuwa na fedha taslimu. Faida ya kampuni ni mali ya wanahisa.Ukimiliki hisa unamiliki mali za kampuni pamoja na faida.
Hisa ni aina mojawapo ya kuhifadhi fedha katika mfumo wa akiba.Fedha inayowekwa akiba inaweza kutumika kwa  ajili ya kununua hisa na hivyo kubadilisha muundo wa akiba kutoka fedha taslimu na kuwa katika muundo wa hisa.
Mada hii inaendela,usiache kuifuatilia mpaka mwisho.…..
Wako faraja mmasa a.k.a MOA

***************Tafuta kupata mafanikio kama utaishi milele lakini kumbuka kumcha Mungu wako na kutenda mema kama leo ndio siku yako ya mwisho kuwepo katika Dunia hii*************
Share:

KUHUSU MMILIKI WA BLOG HII

My photo
Naitwa faraja Mmasa a.k.a Moa,Mkazi na mzaliwa wa Wilaya ya Gairo Morogoro.KARIBU KATIKA BLOG hii tuelimishane mambo mbalimbali.Inatupasa kuwa na ufahamu wa mambo mbalimbali ili tuweze kuyatawala Mazingira yetu .Kuwa na Mwanasheria au Mhasibu haimanishi unatikiwa kujua au kufuatilia maswala ya uhasibu na sheria tu.Mfano nyumba yako au ndoa yako hutaindesha kwa taaluma uliyonayo.Vile vile huwezi kuendesha ujasiliamali kwa mafanikio kwa shahada yako ya uhandisi.TUNAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA

UJUMBE WA LEO

MIUJIZA MINGI INAYOTOKEA KATIKA MAISHA IPO KATIKA MAWAZO,FIKRA,NA IMANI ALIYONAYO MWANADAMU HUSIKA

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

GAR AD2

GAR AD2

GARI ADVERT

GARI ADVERT

Castrol

Castrol
Powered by Blogger.