Tuesday, April 22, 2014

UNAWEZA KUJIAJIRI KUPITIA KILIMO CHA VITUNGUU NA KUPATA FAIDA KUBWA




Mwaka uliopita niliandika makala kuhusu wasomi kujifunza kujiajiri nilikusudia kuwasilisha ujumbe mmoja ya kwamba, “Wasomi na watanzania kwa ujumla wetu tunatakiwa kubadilisha mitazamo yetu ili kujipatia mipenyo ya kiuchumi na kifedha (financial freedom.
Kimsingi ni kwamba zipo imani zinazosapoti watu kuwa na fedha za kutosha na zipo imani na mitazamo inayozuia watu kuwa na fedha ama inawafanya waishi maisha ya kupungukiwa nyakati zote! Imani na mitazamo hii kimsingi huzalishwa kutokana na malezi, utamaduni na mazingira. Mtazamo wa mtu kuhusu fedha tunaita, “Money blue print” .
Nafahamu kuwa wengi kama sio wote tunakubaliana kuwa fedha zina umuhimu mkubwa sana katika maisha ya mtu, na kwamba ukosefu wa fedha ndio msingi wa maovu(Ingawa wapo watu wanatumia fedha kufanya uovu wao) tunachotofautiana ni imani kuhusu fedha. Mitazamo kuhusu fedha ndio inayoamua kiwango cha fedha alichonacho kila mmoja. Hii ina maana kuwa kila mtu anamiliki kiwango cha pesa sawa sawa na imani ama mtazamo wake kuhusu fedha.
vitunguu
Miaka michache iliyopita wakulima walikuwa ni watu wanaotazamwa kama watu wenye shida, walio jitokeza kuwekeza kwenye kilimo walionekana wameshindwa shule ( waliokimbia umande). Na hii ilisababishwa na imani ama mapokeo ya tuliyolishwa na wazazi wetu na walimu wetu kutoka kwenye kipindi cha zama za viwanda (Industria Age). Lakini kwa sasa dunia imebadilika sana, kilimo kimewafikisha watu kwenye ndoto zao, Nimesoma kwenye jarida la Forbes kwamba tajiri wa kwanza Afrika amewekeza kwenye kilimo, wajarisiamali wakubwa hapa Tanzania wamewekeza kwenye kilimo, na wale wanaojiona wameenda shule ‘middle class’ wanaendelea kushangaa na kuendelea kuongea sentensi hasi na kulalamikia viwango vidogo vya mishahara.
  Miaka ya hivi karibuni kwenye Mikoa ya Arusha, Manyara, Iringa, Mbeya,Tanga, Singida na Kilimanjaro zao la vitunguu limejizolea umaarufu mkubwa kwa kuendelea kuajiri maelfu ya Watanzania. Kuna ambao wamefikia ndoto zao kupitia kilomo cha vitunguu, wamejenga nyumba, wamefungua makampuni yao, wanasomesha watoto nk. Vitunguu hivi hivi kuna rafiki zangu wamenunua magari ya ndoto zao, wamejipa likizo nchi za nje.

Share:

KUHUSU MMILIKI WA BLOG HII

My photo
Naitwa faraja Mmasa a.k.a Moa,Mkazi na mzaliwa wa Wilaya ya Gairo Morogoro.KARIBU KATIKA BLOG hii tuelimishane mambo mbalimbali.Inatupasa kuwa na ufahamu wa mambo mbalimbali ili tuweze kuyatawala Mazingira yetu .Kuwa na Mwanasheria au Mhasibu haimanishi unatikiwa kujua au kufuatilia maswala ya uhasibu na sheria tu.Mfano nyumba yako au ndoa yako hutaindesha kwa taaluma uliyonayo.Vile vile huwezi kuendesha ujasiliamali kwa mafanikio kwa shahada yako ya uhandisi.TUNAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA

UJUMBE WA LEO

MIUJIZA MINGI INAYOTOKEA KATIKA MAISHA IPO KATIKA MAWAZO,FIKRA,NA IMANI ALIYONAYO MWANADAMU HUSIKA

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

GAR AD2

GAR AD2

GARI ADVERT

GARI ADVERT

Castrol

Castrol
Powered by Blogger.